AMKA JITAMBUE

 

Robison Robison Author
Title: AMKA JITAMBUE
Author: Robison
Rating 5 of 5 Des:
AMKA JITAMBUE.. Karibu mpenzi msomaji karibu katika blog hii, ambapo tutapata fursa za kujifunza na kukumbushana mambo ya msingi kabisa yana...
AMKA JITAMBUE..

Karibu mpenzi msomaji karibu katika blog hii, ambapo tutapata fursa za kujifunza na kukumbushana mambo ya msingi kabisa yanayo husu maisha yetu, nakufikia kiwango cha mafanikio tunayoyataka. Kila mtu kuna mahali anataka kufika katika maisha yake lakini changamoto ni namna ya kuyafikia malengo yako. Nini mifanyike ili uweze kufika mahali unapo pataka.

Kitu kikubwa kinachoweza kubadilisha maisha yako kabisa ni TAARIFA na MAARIFA ukiweza kupata taarifa sahihi  basi uwe na uhakika utapata maarifa ambayo yatakusaidia kujua ufanye nini na kwa wakati gani. Ukishindwa kutambua nyakati basi kila kitu utakua unakifanya nje ya muda sahihi na matokeo take hayawezi kuwa mazuri.

Lengo ni kuhakikisha tunakupa taarifa sahihi zinazohusu kufikia ndoto zako kimaisha. Watu wengi wanakwama kwasababu hawana taarifa sahihi za kibiashara, kiuchumi, kijamii na kisakologia. Ili uweze kushinda katika dunia ya sasa ni lazima uwe na wingi wa taarifa kwenye akili yako kuliko watu wengine hasa katika eneo lako la kutafutia kipato.

Jifunze au fuata nyayo za watu walio fanikiwa zaidi yako, utakuta wote wana taafifa muhimu kukuhusu jambo flani, lakini pia siyo wavivu kujifunza vitu vipya kila siku hasa kwenye eneo husika kwenye maisha yao. Chukua tabia hiyo ya kuwa na kiu ya kutaka kupata  maarifa zaidi

Kwanzia sasa ni muda wa ku AMKA pale tulipo jikwaa na ku JITAMBUA tumekosea wapi na nini tukifanye ili kujenga hali ya matokeo chanya kwenye kila jjambo tunalolifanya. Hakuna tabia ya kusikitisha na kukatisha tamaa kama kila jambo unalotaka kulifanya halifanikiwi, au unakutana na vikwazo ambavyo kwa hali ga kawaisa ni vigumu kwako kuviruka. Tuko hapa kukutia moyo na kukuonyesha njia ya kutokea na wewe kufanikiwa.

Jifunze kwa kuanza kufanya vitu vipya katika maisha yako, usisikilize sana hadithi za watu walioshindwa katika maisha yao. Ukitembea na mpumbavu kuna uwezekano mkubwa na wewe kuwa mpumbavu. Enenda na wenye hekima na wewe utakuwa na hekima, sikiliza ushauri wa watu waliofanikiwa kwenye sehemu flani uwe kibiashara ama maisha kiujumla. Ukisikiliza walio feli lazima wataua ndoto yakp ya kutaka kufanikiwa.

Karibu sasa katika safari hii ya kutimiza ndoto zetu, hatua kwa hatua tutajifunza ni kwa namna gani tunaweza kutengeneza aina ya maisha tunayoitaka. Kwasababu mifano ya watu walio fanikiwa ipo kwanini wewe ushindwe, hakuna bahati katika kufanikiwa ila kuna vitu ambavyo ikivifanya na ukavifatia kwa umakini mafanikio tatakuwa ni yako.

Usikubali kuushi maisha ha ukawaida, tafuta utofauti usiwe mwepesi kulidhika. Kuwa na ndoto kubwa katika maisha yako usikubali kushindwa mpaka lengo lako litimie haijalishi upo katika hali gani wakati ulionao ilikufanikisha ndoto zako ni sasa. Anza leo kutekeleza ndoto zako amza sasa kuandaa maisha unayo yataka kesho.

KARIBU....
09 Mar 2016

About Author

Advertisement

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top