AMKA JITAMBUE

 

Robison Robison Author
Title: STUKA LEO
Author: Robison
Rating 5 of 5 Des:
  “Kwanza unatakiwa kujitambua wewe ni nani”, hii ni kanuni ya kwanza kabisa niliyo inukuu kutoka kwa mkuu wa mkoa wa Dar e...






 Image result for rich people image

“Kwanza unatakiwa kujitambua wewe ni nani”, hii ni kanuni ya kwanza kabisa niliyo inukuu kutoka kwa mkuu wa mkoa wa Dar es Saalam, Mh Paul Makonda. Katika kujijua na kujitengenezea fursa wewe mwenyewe ni lazima kwanza ujitambue wewe ni nani. Bila kujua wito wako utahangaika miaka yote ukijaribu kufanya kila jambo na kuona haliendi au haalisogei na kuto kuona motokeo ya jitahada zako kwasababu moja tu unafanya kinyume na wito wako. Ni lazima ufike mahali ujitambue wewe upo hapa duniani kufanya nini?

Ishara moja kubwa ya kutambua mahali ulipo ni sahihi au siyo sahihi ni matokeo ya kile unacho kifanya kuna watu wengi wamesoma na wanafanya kazi kupitia elimu zao lakini huduma anayo itoa haifurahishi au haina ubora kabisa hata kama viwango vyake vya elimu ni vikubwa, hili ni tatizo kubwa hapa inchini kwetu tunavijana wengi walio soma lakini hatupati matokeo mazuri ya elimu zao kutokana na ukweli kwamba walichosomea siyo wito wao wanafanya tu kwasababu ya  pesa.
Stuka mapema leo tambua uelekeo wako, tambua lengo lako la uwepo katika hii dunia hakika hujachelewa wakati ni sasa chukua hatua ya kujigundua wewe mwenye na chukua hatua za kutimiza ndoto zako, najua hata wewe mpenzi msomaji unafahamu umuhimu wa mtu kugundua kipaji chake na namna gani kipaji kinavyo kuwa na uwezo wa kubadilisha maisha ya mtu, sasa kwanini huchukui hatua na kutafuta nafasi ya kutumia kipaji chako.

Tatizo ni fikra, na mtazamo ulionao. Ukitaka kuelewa hapa namaanisha nini jiulize swali hili ukisikia swala la kutambua kipaji akili yako inaona ni swala gumu au swala rahisi. Kama bado hujagundua uwezo wako dhahiri lazima utakuwa unaona ni jambo gumu sana na haliwezekani kirahisi labda mpaka atokee mtaalamu Fulani mwenye elimu ya juu ndo aje akuonyeshe kipaji chako, jibu ni hapa huu mtizomo wako wa kuona kuvumbua hazina ya kipaji chako ni swala gumu ndiyo unao kukwamisha kufikia mafaniko yako. Ukweli ni kwamba kutambua wito wako ni rahisi kuliko kitu chochote kile kwasababu kipaji hicho au wito huo upo ndani yetu hatuna haja ya kuhofu katika hilo.

Changamoto kubwa ni kwamba watu wengi hatuna muda wa kujitathimini, wa kujisoma na kujitafuta sisi wenyewe ila tunakuwa bize zaidi na habari au na maisha ya watu wengine kuliko ya kwetu matokeo yake tunajikuta hatuna muda wakitafakari sisi ni akina nani au wito wetu ni upi, lakini pia hii hali inasabishwa zaidi  na kuishi maisha ya mazoea kwasababu jamii nyingi za kitanzania hazina utaratibu wa kukugundua vipaji au wito wa watoto wao, hivyo basi tabia hiyo inaenda kizazi kimoja kwenda kizazi kingine na inaua kabisa uwezo wa kujitambua.

Ndiyo maana tunakwambia stuka mapema kwasababu katika jamii hizo hizo kuna vijana kama wewe ambao wamekwisha kujitambua na leo hii tunaona makifanya vitu vikubwa taifa na dunia kwa ujumla inatambua uwepo wao, kutokana na vile vitu wanavyo vifanya. Kamwe usijione wewe upo katika hali ngumu sana kimaisha na huwezi kufanya lolote au huna tena nafasi ya kufanikiwa, kwasababu njia bado zipo nyingi za kukutoa hapo ulipo na wewe kukuza ndoto yako na kufanikiwa, wapo watu wengi walio kuwa na hali kama yako, lakini leo hii wanaongea lugha ya tofauti kabisa lakini ni baada ya kustuka mapema na kuchukua hatua, wakati wako ni sasa.

Kamwe usikubali kuwa mtu wa kawaida kwamaisha yako, kwasababu hukuletwa hapa duniani kuja kuzurura na kuwa mtu wa kawaida, hivyo basi kwanzia leo jiwekee viwango vya kimaisha unavyo vitaka, jione ukiwa umefanikiwa na mwenye furaha kupitia kile unacho kifanya. Kubali kukabili changamoto zote hakuna wa kukumisha wewe kufikia ndoto yako, unachotakiwa tu ni kustuka mapema na kusonga mbele kutimiza ndoto yako
 Image result for rich people image

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top