lakini inabidi ufanye mamba kadhaa huwezi kufikia kiwango hicho bila kuwa tayari kufata kanuni zake.
kwanza kabisa ni lazima uwe tayari kulipa gharama za huo utajiri unaoutaka safari ya kuutafuta utajiri siyo nyepesi ni lazima utoae vitu kadhaa, uache kuona aibu, uwe jasiri, ujitume zaidi, upunguze anasa na uongeze saving nk.
siri ya kwanza kabisa ili uweze kuwa tajiri ni lazima ujifunze kuweka akiba, bila fedha ya ziada huwezi kuwekeza mpango mkakati wa kwanza anza kujibana na kuweka akiba ili uweze kuwekeza.
pili anza kutafuta mradi au tafuta vyanzo vingine vya mapato, kamwee usiishi kwa kutegemea chanzo kimoja cha mapato utakwama, anza kujiwekeza fungua miradi mingi kwa kadri utakavyo weza.
saidia wengine, usiwe mchoyo mtolee MUNGU wako kwa misingi ya imani yako lakini pia saidia wengine hapo lazima utaona mpenyo wa kiutajiri ukikujia katika maisha yako.
tafuta maarfa, ukitaka kufanikiwa kuwa makini sana na mambo unayo jifunza, siyo unataka utajiri lakini hakuna uanchokisoma kuhusu biashara na uwekezaji ujue unajifurahisha tu huwezi fika popote. tafuta maarifa ya kiutajiri utakuwa tajiri.
sambamba na hayo tenga muda wa kutafakari, mtu tajiri anakuwa na muda wa kujitathimini na kupanga mikakati mipya pale inapo bidi.
kwanzia sasa anza kujifikiria kama tajiri, na lazima utakuwa tu.
Post a Comment