AINA TANO ZA MITAJI
Na Robison
Sisyan
Watu wengi
tunashindwa kufanya vitu katika maisha yetu kutokana na ukweli kwamba tunalia
hatuna mitaji, siyo hivyo tu watu wengi wamekwisha sema ukisema unatafuta mtaji
ujue wewe ndiyo mtaji wa kwanza. Sasa wewe unwezaje kuwa mtaji au ni kitu gani
kinakufanya wewe uwe mtaji.
Leo tutajua
sababu ambayo inakufanya wewe uitwe ni mtaji wa kwanza na unaposema unatafuta
mtaji ujue unajitafuta wewe mwenyewe na kujua tu unatumiaje ulivyo navyo ili
kufanikiwa katika maisha yako.
Kiu yetu ni
kuona mafanikio katika maisha yetu, lakini kwenye hii safari ya kufikia malengo
yote, kuna vitu tunajikuta hatua, na hivi vitu huwa ni muhimu sana kufikia
malengo yetu, kimoja wapo ni kujitambua. Ukijitambua wewe ni nani uko wapi, na
unatakiwa kufanya nini.
Zifuatazzo
ni aina za mitaji ambazo kila mwanadamu anazo, kinachotakiwa ni kuzitambua na
kuanza kuzianyia kazi ili zikuletee matokeo mazuri.
Uhai, kama
unasoma makala hii, ujue unanafasi ya kufanikiwa katika maisha yako, mtaji wa
kwanza ni uhai, huwezi kufanya jambo lolote ukiwa ni maiti, ukiwa hai ndiyo
uaweza ukafanya na ukatenda na vitu vikatokea, hivyo huna budi kujikita katika
kuthamini uhai wako kwa kuutumia ipasavyo ili uweze kufanikiwa.
Afya, mtu
mwenye afya njema anauwezo wa kushiriki shughuli yoyote ya uzalishaji na kwa
ukamilifu, ukiwa hauko timamu kiafya huwezi kutekeleza majukumu yako hata ukiwa
na nia ya kufanya hivyo, hivyo basi afya tulizo nazo ni mtaji tosha kwasababu
tunaweza tukaamua cha kufanya kwa wakati wowote na kikawa.
Akili, mtaji
mwingine ni akili, hapa tunazungumzia utashi, uwezo wa kutambua na kuelewa,
wewe ni nani uko wapi, na unatakiwa ufanye nini, kwenye akili ndiko kwenye
hazina ya majawabu ya maswali yetu. Ili akili ipate nafasi ya kufanya kazi
vizuri ni kazima iwe na maarifa, kazi
unayotakiwa kuwa nayo katika maisha yako ni kujaza akili yako maarifa ya
kutosha.
Uwezo wa
kufikiri, kila mtu kajaliwa uwezo wa kufikiria, kwenye kufikiria kwa ufasaha na
kwa ufanisi kunahusisha zaidi akili yenye maarifa. Mtu anae jua kufikiri vizuri
ni lazima ajue kupanga na kweka mikakati dhidi ya maisha yake mwenyewe, huwezi
kufanikiwa kama hutengi muda wa kufikiri na kuweka malengo katika maisha yako,
swala ni wewe kuamua kuanza kufikiria ili upate jibu la matatizo yako.
Uwezo wa
kuamua, ulichokifikiria katika akili yako ilikitokee ni lazima ufanye maamuzi
ya kuchukua hatua ya kuyatekeleza, usiishe kuwaza na kufikiria pekee chukua
hatua na kuyatekeleza maamuzi yako. Hapa kwenye kuamua ndiyo kwenye utendaji
anza na kile ulichonacho kukamilisha mawazo yako ili kufikia ndoto yako.
Huu ndiyo
ukweli na hazina zilizo jificha katika maisha yetu, hii ni mitaji na ndiyo
nguzo kuu za mafanikio, hakuna mafanikio yanayotoka nje ya haya mambo matano na
ukisha jua jinsi ya kuyatumia haya ndipo utakapo jigeuza wewe mwenyewe kuwa
mtaji, lakini pia ndipo utakapo jigeuza wewe mwenyewe kuwa mtaji na kuweza
kuzalisha mali na utajiri katika maisha yako.
Amkajitambue.blogpot.com
+255 653 206
053
Post a Comment